Monday, September 1, 2008

Miaka 44, Bravo JWTZ.

Thomas Mushi
Dar es salaam September 1 2008 JWTZ………..
Jeshi la wananchi wa Tanzania limeadhimisha miaka 44 tangu kuanzishwa kwake kwa kuahidi kuendelea kutekeleza kwa vitendo madhumuni ya kuundwa kwa jeshi hilo likiwemo jukumu la ulinzi wa nchi na utoaji wa huduma kwa raia wakati wa dharura.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na waziri wa ulinzi wa Comoro Mohamed Bacar Dosar na Mkuu wa Majeshi wa Comoro Brigedia Jenerali Salimoo Mohamed ambao wamelikushukuru jeshi la wananchi wa Tanzania kwa kufanikisha kumuondoa madarakani kiongozi muasi Kanali Mohamed Bacar katika operesheni ya kijeshi visiwani Anjouan.

Viongozi hao pia walitoa mkono wa pole kwa wajane wa askari wawili wa Tanzania waliofariki dunia nchini Comoro. Askari hao ni Coplo Rafael Sarakikya kutoka Arumeru Arusha aliekufa maji siku mbili kabla ya kuanza kwa operesheni hiyo wakati PRIVATE Hamis Makame kutoka kaskazini Unguja alifariki dunia kwa kuugua siku chache baada ya kumalizika kwa opesheni hiyo.

Akizungumza katika hafla fupi Makao makuu ya jeshi upanga jijini Dsm, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dr Hussein Mwinyi amesema,jeshi la wananchi wa Tanzania linajivunia rekodi yake ya mafanikio makubwa katika operesheni zake wakat wa amani na zile za kivita ambazo zimeiuletea nchi heshima kubwa

Akizungumzia hoja ya kuwataka askari wa jeshi hilo kulipa nauli katika vyombo vya usafiri, waziri Mwinyi amesema, chombo chenye maamuzi ya kutangaza agizo hilo ni Sumatra, baada ya kufanya mashauriano na wadau. Ameongeza kuwa, kufuatia ukimya wa Sumatra katika suala hilo, ni wazi kuwa bado majadiliano hayakamilika hivyo watoa huduma wasubiri agizo la Sumatra na si vinginevyo.

Kuhusu mafanikio makubwa ya opesheni Democracy Comoro iliyofuatiwa na ahadi ya Rais kuwapa nishani askari walioshiriki,mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Jenerali Mwamunyange amesema, nishani hizo zinaandaliwa na zitakapokuwa tayari umma utajulishwa.

Katika vuwanja vya Jeshi, Mkuu wa majeshi jenerali Davis Mwamunyange na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi Luteni Jenerali Abdurahman Shimbo wamewaongoza maafisa, askari na wananchi katika sherehe hizo ambapo wimbo mpya wa jeshi ulizinduliwa rasmi baada ya mchakato mkali uliosimamiwa na wataalamu

End……..

No comments: